Monday, 10 November 2014

Watumishi sekta ya afya waungana na wakunga wa jadi

Watumishi wa sekta ya afya katika halmashauri ya wilaya ya Nkasi Mkoani RUKWA wameandaa mpango maalumu wa kushirikiana na wakunga wa jadi katika wilaya hiyo ili kukabilina na changamoto za vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua.
Akizungumzia mpango huo mganga mkuu wa hamlashauri ya wilaya ya Nkasi DKT GWAMAKA MWABULAMBO amesema hatua hiyo itasaidia kujenga uelewa kwa wakunga wa jadi namna ya kutumia njia sahihi za kuzuia vifo wakati wa kijifungua na kuwahamasisha mama wajawazito kujifungulia katika vituo vya afya.

DOKTA GWAMAKA amesema wamefikia maamuzi hayo kutokana na ukweli kuwa bado wakunga wa jadi wanaendelea kutumiwa kuwazalisha mama wajawazito na hasa katika baadhi ya maeneo yaliyo mbali na huduma za afya kikao cha pamoja kitasaidia kuwaelimisha wakunga hao wao kuwa msaada wa kuwapeleka akina mama hao maeneo mahususi kwa ajili ya kujifungua salama.

0 comments:

Post a Comment