Wednesday, 12 November 2014

Mradi wa maji SBL kunufaisha Temeke

SEKTA ya afya nchini imezidi kupata msukumo baada ya kuzinduliwa kwa mradi wa maji katika zahanati ya Mkamba, Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam.

Mradi huo uliozinduliwa jana ulifanikiwa baada ya uwekezaji wa sh. milioni 50 uliofanywa na kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL).

Kutokana na mradi huo, pia zaidi ya wakazi 80,000 wa Mkamba, sasa watafaidika na maji safi na salama uliotekelezwa katika mradi wa kampuni hiyo wa “Maji kwa Uhai”.

Mradi huu unajumuisha kisima cha maji, tenki la maji na pampu inayotumia umeme wa jua na lina uwezo wa kuzalisha hadi lita 4,000 za maji kwa siku.

Pia utasaidia katika kuwezesha utoaji huduma endelevu na shughuli nyingine katika zanahati ya Mkamba ambayo hapo awali lilishindikana kuzinduliwa kutokana na tatizo la uhaba wa maji masafi na salama.

"Tunafurahia kuwa kati ya wadau ambao wamechangia kutoa suluhisho la changamoto ya uhaba wa maji,” alisema Mkurugenzi Mtendaji wa SBL, Steve Gannon.

Kabla ya mradi huo, upatakinaji wa maji safi na salama katika zahanati hiyo ilikuwa changamoto, na hali hiyo ilisababisha kuchelewa kwa ufunguzi wa zanahati.

Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sofia Mjema, ambaye alikuwa mgeni rasmi alisema kukamilika kwa mradi huo katika kituo cha afya cha Mkamba ni moja ya hatua muhimu za kuboresha huduma za maji katika hospitali nchini.

0 comments:

Post a Comment