Friday, 7 November 2014

Waliowekwa karantini kuachiliwa wiki ijayo


Zaidi ya watu 100 waliotengwa nchini MALI kwa kuhofiwa kuwa wameambukizwa ugonjwa wa EBOLA wataachiwa huru wiki ijayo baada ya kukamilisha siku 21 za uchunguzi.
Watu hao ni pamoja na ndugu na wauguzi waliokuwa karibu na mtoto mmoja wa miaka MIWILI aliyefariki dunia nchini MALI kwa ugonjwa wa EBOLA.

Mtoto huyo alikuwa amesafiri kwa basi kutoka nchi jirani ya GUINEA akiwa na dalili ya ugonjwa huo wa EBOLA. Tarehe 23 mwezi Octoba nchini ya MALI ilitangaza kuwa ina mgonjwa mmoja wa EBOLA.

0 comments:

Post a Comment