
Idadi ya wanawake wanaokwenda hospitali kujifungua imeongezeka Mkoani
MBEYA ikilinganishwa na miaka MITATU iliyopita baada ya kuanza
kutekelezwa kwa mradi wa matibabu bure kwa wajawazito mkoani huo.
Mganga Msaidizi katika Hospitali ya Rufaa ya MBEYA Kitengo cha
Wazazi cha META Dakta GODLOVE MBWANJI amesema hayo mbele ya maafisa wa
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya waliofanya ziara ya kushitukiza katika
hospitali hiyo kuangalia namna mradi wa matibabu bure kwa wajawazito
unavyotekelezwa.
Mradi wa matibabu bure kwa akinamama wajawazito ulianzishwa mwaka
2012 kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Watu wa UJERUMANI na tayari
wanawake zaidi ya LAKI MOJA NA ELFU 70 wa Mikoa ya TANGA na MBEYA
wamenufaika na huduma hiyo ambapo pia umepunguza vifo vya akinamama
wajawazito.



0 comments:
Post a Comment