![]() |
| Lewis Hamilton |
Nguli wa zamani wa dunia wa mbio za
magari Nigel Mansell amesema Lui Hamilton anayo nafasi moja iliyosalia
kufanya vyema na kutinga fainali huko Abu Dhabi November 23.
Hamilton anaiongoza timu ya Mercedes kwa pointi 17, na nafasi ya kufanya maajabu anayo mikononi mwake.
Awali ni awali ,mwaka 1986 huko Australia kwenye
Mbio za Langa langa zilishuhudia William akiukosa ushindi hivi hivi baada ya kupata pancha . lakini yeye anasema hana tofauti na bata, mzoefu wa kupata,!
Alisahau maumivu ya tairi kukosa upepo na kuukosa ushindi pale alipojiona ana bahati ya mtende kuota jangwani baada ya kupata tuzo ya Sports Personality of the Year zitolewazo na BBC kakosa huku kapata kule!
Kama wewe ni shabiki sugu wa michezo!Tuzo hizo zimewadia tena ingia katika mtandao wa BBCSWAHILI.COM utapata maelekezo ya namna ya kupiga kura kumchagua mchezaji umtakaye, akwae tuzo hiyo ya BBC SPORTS PERSONALITY OF THE YEAR, na Mshindi atatangazwa baadaye mwezi ujao kazi kwako.




0 comments:
Post a Comment