Mtaalamu wa masuala ya mabadiliko ya tabianchi nchini BRAZIL amesema
kuna uhusiano mkubwa kati ya uharibifu wa mazingira katika msitu wa
AMAZON na mfululizo wa ukame nchini humo.
Dr. ANTONIO NOBRE amesema takwimu zinaonyesha kuwa ukame huo umekuwa na madhara makubwa katika mji SAO PAULO nchini BRAZIL.
NOBRE amesema vyanzo vya maji vinaweza kutoweka na kusababisha
madhara kwa zaidi ya watu milion 20 iwapo hali hiyo ya uharibifu katika
msitu wa AMAZON haitadhibitiwa.
Baada ya ukame kwa zaidi ya miaka MINANE mfululizo kina cha maji
katika huo wa SAO PAULO kipo hatarini. Serikali nchini humo iansema
imelazimika kuanzisha mgao wa umeme kutokana na uhaba wa maji ikiwa ni
moja ya hatua za dharura .



0 comments:
Post a Comment