Bei ya mbuzi na kondoo jijini DSM imepanda maradufu kutokana na mahitaji makubwa ya wanyama hao kwa ajili ya sikukuu ya EID EL-HAJI itakayofanyika siku ya jumapili 05/10/2014 ambapo muumini wa dini ya kiislamu anatakiwa kuchinja mnyama
Katika soko la mbuzi la Vingunguti , bei imepanda kutoka shilingi elfu sitini kwa mbuzi au kondoo mmoja hadi shilingi laki moja na ishirini ambapo baadhi ya wachuuzi wa soko hilo wamesema mauzo yameongezeka kutokana na mahitaji makubwa ya wanyama hao.
Hata hivyo wateja wa soko hilo wamesema bei hiyo ni kubwa kupita kiasi jambo ambalo linaweza kusababisha baadhi ya waislamu kushindwa kutimiza ibada muhimu ya kuchinja



0 comments:
Post a Comment