Wafugaji wa wilaya za Longido na Monduli Mkoani Arusha wameiomba Serikali na wadau wengine kuwajengea uwezo wa Kufuga aina za mifugo wenye tija na wanaohimili ukame ikiwemo Mbuzi, Kondoo na kuku kama hatua ya kukabiliana na Mabadiliko ya Hali ya Hewa ambayo yanaendelea kuwaathiri siku hadi siku.
Wakizungumza na watendaji wa Mtandao wa vikundi vya wakulima na wafugaji nchini (mviwata) waliotembelea Baadhi ya Vikundi wananchi hao wamesema pamoja na misaada wanayopata wanaendelea kukabiliwa na umaskini kutokana na athari za ukame hivyo wameshauri kuwezeshwa kufuga mifugo inayohimili hali iliyopo.
Baadhi ya wanawake walianza kufuga mbuzi ,na kuku wamesema aina hiyo ya Mifugo inaweza kuwapunguzia makali ya maisha kama watasaidiwa kuepukana na Magonjwa na hivyo kuwezeshwa kufuga kibiashara.
Afisa ugani kutoka Mtandao wa wakulima (mviwata ) mkoa wa arusha Bi,Eunoti Aberenego Amesema Baada ya kufanikiwa kuwahamasisha wafugaji na wakulima kuunda vikundi sasa wanaendelea kuwaelimisha juu ya umuhimu wa kulima na kufuga kwa tija japo bado kuna changamoto kubwa ya aina za mbegu za Mifugo na mazao ya chakula.
Baadhi ya viongozi akiwemo Diwani wa kata ya namanga Bw John Kimli amesema asilimia kubwa ya Ng”ombe wameshaanza kuathirika na ukame licha ya kuwashukuru wadau wanaendelea kuwasaidia kwa kuwapa Mbegu za Ng”ombe wa kisasa zikiwemo zilizotolewa na Mh.Rais ,ukame umeziathri kwa kwa Kiasi kikubwa.




0 comments:
Post a Comment