Baadhi ya watumishi wa mamlaka ya maji ya Mji mdogo wa Usariver wilayani Arumeru wamelalamikiwa kushirikiana na Baadhi ya watu kuhujumu miundombinu ya maji ili waweze kujipatia fedha wakati wanapohitajika kutengeneza Miundombinu hiyo.
Malalamiko ya hujuma hizo ikiwemo ya kukata mabomba yametolewa na wananchi wa mji huo ambao wamesema hatua hiyo pamoja na kuwaongezea makali ya tatizo la maji inawasabibishia Hasara.
Akizungumzia malalamiko hayo Meneja wa mamlaka hiyo Bw, Daniel Ndeku amekiri kupokea malalamiko hayo na tayari ameshaanza kuyafanyia kazi na ameongeza kuwa pia lipo tatizo la wakandarasi wanaopewa kazi ya ujenzi wa barabara kutojali Miundombunu ya maji.
Baadhi ya watendaji wa sekta ya barabara wamesema tatizo la ukataji wa mabomba ya maji wakati wa kukarabari Barabara linatokana na utaratibu wa baadhi ya wananchi wa kutofuata taratibu wakati wa kuunganishiwa huduma ya maji.



0 comments:
Post a Comment