Wednesday, 1 October 2014

WANAFUNZI WA CHUO CHA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI ARUSHA WAPEWA SEMINA YA UJASIRIAMALI.

 Na, Seif Baruti.

Mkurugenzi wa chuo cha uandishi habari na utangazaji Arusha Bw. Joseph Mayagila amefungua semina ya ujasiriamali hii leo  itakayomalizika siku ya ijumaa chuoni hapo.

Bw. Joseph Mayagila aliesema kuwa semina hiyo ni muhimu sana kwa wanafunzi wote kwa sababu dunia ya sasa imejengeka katika misingi ya ujasiriamali na ili mtu yeyote afanikiwe kibiashara ni lazima ajue kupanda mbegu, thamani ya muda pamoja na mavuno ambayo ni matokeo ya kupanda mbegu.
Mkurugenzi wa mafunzo katika chuo cha uandishi wa habari na utangazaji akifungua semina ya ujasiamali mapema leo: picha BENSON MREMI

Semina hiyo iliyowahusisha wanafunzi wa kozi zote chuoni hapo ikiwemo kozi ya Uandishi wa  habari na Utangazaji, Ualimu,Sekretari pamoja na kozi ya Kompyuta.

Katika semina hiyo ziliawasilishwa mada kuu tatu na Wakufunzi wa Chuo hicho, ambapo mwalimu Onesmo Elia Mbise aliwasilisha mada ya mikakati ya kibiashara,  na mada ya huduma kwa wateja iliwasilishwa na Bw, Christian Ndege nae Mratibu wa semina hiyo Bw. Adrea Ngobole aliweza kuwasilisha mada ya misingi au mikakati ya mjasiriamali.

Mbise alisema mjasiriamali anatakiwa kuwa na mikakati mahususi kuhusu biashara anayofanya kwa kuweza kujiuliza maswali ya msingi na kujijibu katika biashara yake ili kuweza kutatua changamoto  zitakazo mkabiri mfabiashara huyo.

Mfanyabiashara anatakiwa kuwa na wazo la kibiashara ambalo familia yake imekubaliana nalo ili iweze kumsaidia pindi anapohitaji kutumia baadhi ya rasilimali za familia  kuwa rahisi kwake kuzipata, pia anatakiwa kuwa ni mtu mzuri wa matuminzi ya muda na awe tayari kufanya kazi kwa bidii zaidi ya yule aliyemwajiri, alisema Mbise

Mkufunzi katika chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha Bw. Onesmo Mbise akiwasilisha mada leo: picha BENSON MREMI

 Bw, Christiani Ndege katika uwasilishaji wake wa mada ya pili alisema, mjasiriamali anatakiwa kuijua vizuri biashara yake ili aweze kumbakiza mteja wake kwa kumtafutia mbadara ya bidhaa aliyokuwa anaihitaji pindi anapoikosa katika biashara yake.

“Wafanyabiashara wengi huwapoteza wateja wao bila ya wao kujijua, kwani mteja ni rahisi kumpata ila ni vigumu sana kumfanya adumu kuwa mteja wako kama hautojua ninamna gani ya kuweza kumfanya awe wako”alisema Ndege

Mfanyabiashara anatakiwa kuwa na lugha nzuri kwa mteja wake ili kumfanya ajisikie kuwa yeye ni wa dhamani kwake, pia wafanye wateja wako  wafahamu mfumo unaotumia na kumsaidia mteja kufaniksha huduma anayoitaka na uumpe mteja wako kitu cha ziada na alichokuwa akikihitaji.

Nae, Bw. Adrea Ngobole alisema mjasiriamali anatakiwa kuwa na wazo tajirishi na awe na jicho la kuona fursa ambazo zinapatikana mbele ya jamii kwa kuweza kutoa majibu ya changamoto yanayopatikana katika jamii hiyo.

Pia Mjasiriamali  anatakiwa kuweka mipango endelevu ya kibiashara ili kuweza kumfikisha kuwa tajiri na kuwa mvumilivu kwa matatizo yatakayo mkumba katika biashara yake, pia anatakiwa kuwaepuka marafiki wanaoweza kumkatisha tamaa pindi anapohitaji ushauri, alisema Ngobole.
Mratibu wa semina ya ujasiriamali katika chuo cha uanndishi wa habari na utangazaji Arusha Bw. Andrea Ngobole akitoa mada mapemaa  leo: picha BENSON MREMI

Mmoja wa wanafunzi chuoni hapo,aliyejitambulisha kwa jina la Ziara Nyatu alisema wamefurahi kupata mafunzo hayo kwani yatawawezesha kujiajiri wenyewe pindi wamalizapo mafunzo ya uandishi na hata wakiwa chuoni hapo, licha ya kusubiria kujiajiri ili kujikwamua katika dibwi la kukosa ajira na ana tegemea makubwa katika siku mbili zilizo baki.


Baadhi ya wanafunzi waliohudhuria semina ya ujasiriamali katika ukumbi wa chuo cha uandshi wa habari utangazaji Arusha leo: picha BENSON MREMI





  

0 comments:

Post a Comment