This is default featured post 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured post 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured post 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured post 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured post 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Tuesday, 27 October 2015

MBATIA AMLAZA CHALI MZEE ELYIATONGA MREMA JIMBO LA VUNJO


Mbunge mteule wa jimbo la vinjo Mh. JAMES MBATIA
Tume ya Uchaguzi (NEC) imemtangaza James Mbatia wa NCCR Mageuzi kuwa mbunge mteule wa jimbo la Vunjo huku kada wa Chadema, Anthony Komu naye akiibuka mshindi katika jimbo la Moshi Vijijini lililokuwa linaongozwa na Waziri wa zamani wa Biashara na Viwanda, Dk. Cyril Chami kupitia CCM.

Akitangaza matokeo ya majimbo hayo mawili mkoani Kilimanjaro kuamkia leo, msimamizi Fulgence Mponji, amesema Mbatia amepata kura 60,187 akiwashinda wapinzani wake; Innocent Shirima wa CCM aliyepata kura 16,617 na Augustine Mrema wa TLP aliyepata kura 6,416.

Kutokana na matokeo hayo,  Mrema ameshindwa kutetea kiti chake cha ubunge katika jimbo la Vunjo huku wananchi wa eneo hilo wakiendeleza historia ya kutomchagua mbunge wa chama kimoja kwa vipindi viwili tangu kurudi kwa mfumo wa siasa za vyama vingi.

Kwa upande mwingine, CCM imepoteza jimbo la Moshi Vijijini kupitia kwa mgombea Cyril Chami na kurudi tena upinzani baada ya kada wa Chadema, Anthony Komu kutangazwa mshindi. Hata hivyo, waziri huyo wa zamani wa Viwanda na Biashara hakuwepo wakati NEC wa kusaini kuonyesha kuwa amekubali matokeo.

Kwa mujibu wa Mponji, mbunge mteule wa Moshi Vijijini, Komu amepata kura 55,813 huku Dk Cyril Chami akijikusanyia kura kura 24,415.

MAWAZIRI WA JK WLIOANGUKA KWENYE NAFASI YA UBUNGE MWAKA HUU 2015



Mawaziri watano wa Serikali inayomaliza muda wake wameanguka kwenye uchaguzi majimboni mwao, sambamba na wagombea wengine maarufu wa Bunge lililopita baada ya matokeo ya kura zilizopigwa Jumapili kuanza kutangazwa jana.

Mawaziri hao wanaungana na wabunge wengine maarufu wa Bunge la Kumi walioshindwa kutetea majimbo yao, wakiwamo wa kambi ya upinzani ambao wameangushwa na wagombea wa CCM.

Pia wamo mawaziri wa zamani wawili, Cyril Chami na Omary Nundu walioanguka kwenye uchaguzi, kwa mujibu wa matokeo ambayo yanaendelea kutangazwa.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema jana kuwa itakamilisha kazi ya kutangaza matokeo yote keshokutwa.

Mawaziri walioanguka kwenye uchaguzi huo ni Steven Wasira, Christopher Chiza, Aggrey Mwanri, Dk Steven Kebwe na Anne Kilango.

Katika matokeo yaliyotangazwa jana, Wasira, kada maarufu na mwanasiasa mkongwe aliyekuwa akitetea Jimbo la Bunda, alijikuta akiangushwa na mwanasiasa kijana, Ester Bulaya, ambaye alihamia Chadema baada ya Bunge la Kumi kumaliza muda wake.

Wasira, ambaye alikuwa Waziri wa Kilimo na Chakula, alianza mchakato wa uchaguzi mwaka huu kwa kuomba ridhaa ya CCM agombea urais, lakini hakupitishwa. Bulaya, ambaye alikuwa mbunge wa viti maalum (CCM), alipata kura 28, 508 na kumuacha mbali waziri huyo mkongwe aliyepata kura 19, 126.

Mwingine aliyeanguka ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu- Uwezeshaji na Uwekezaji, Christopher Chiza ambaye ameangushwa na Bilago Samson wa Chadema katika Jimbo la Buyungu. Waziri huyo alizidiwa kwa kura 104 baada ya Samson kupata kura 23,041 dhidi ya 22,934 za Chiza.

Lakini hali haikuwa hivyo kwa Naibu Waziri wa Tamisemi, Aggrey Mwanri kwenye Jimbo la Siha. Waziri huyo alizidiwa kwa zaidi ya kura 4,100 na mpinzani wake kutoka Chadema, Dk Godwin Mollel aliyepata kura 22,746.

Katika Jimbo la Serengeti, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Stephen Kebwe pia alijikuta akipoteza nafasi ya kurudi bungeni kwa kura alipoangushwa na Marwa Ryoba wa Chadema. Dk Kebwe alipata kura 39,232, akiwa amezidiwa na mpinzani wake kwa zaidi ya kura 820.

Anne Kilango, ambaye aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Elimu mwaka 2013 baada ya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyosababishwa na kashfa ya Operesheni Tokomeza, ameangushwa na mgombea wa Chadema, Naghenjwa Kaboyoko wa Chadema kwa tofauti ya kura 3,297.

Kilango alipata kura 15,539 wakati mgombea huyo wa Chadema alipata kura 18,836. Pia wabunge maarufu kama Vincent Nyerere (Musoma Mjini), James Lembeli (Kahama Mjini) na Kyisieri Chambiri (Babati Mjini) wameangushwa.

Nyerere, aliyekuwa akitetea kiti cha Musoma Mjini kwa tiketi ya Chadema, aliachwa mbali na mgombea wa CCM, Vedastus Mathayo aliyepata kura 32, 836 dhidi ya 25,549.43 za Nyerere.

Lembeli, ambaye alihamia Chadema muda mfupi baada ya Bunge la Kumi kumaliza muda wake, aliachwa mbali na mfanyabiashara maarufu, Jumanne Kishimba aliyepata kura 47,553 dhidi ya kura 30,122 za Lembeli.

Wednesday, 21 October 2015

mkuu wa majeshi ya ulinzi nchini Jenerali davis mwamunyange aonekana


Jenerali Davis Mwamunyange
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange, (pichani) aonekana katika Kamandi ya Anga Kizuka iliyopo Ngerengere, mkoani Morogoro wakati Rais Jakaya Kikwete, akizindua uwanja wa Ndege wa Kamandi hiyo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Rais Kikwete alisema kuwa katika miaka 10 ya uongozi wake, amefanya mambo mengi kwa Watanzania pamoja na kuliacha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) likiwa katika hali nzuri ya kiutendaji.

Alisema hakuna nchi inayoweza kupata maendeleo mbalimbali kama haina jeshi imara kutokana na kuwapo vitendea kazi vya kutosha na madhubuti vinavyoimarisha jeshi hilo.


Jenerali Mwamunyange alisema katika kipindi chote cha uongozi wa Rais Kikwete, ameimarisha JWTZ na kutimiza mahitaji ya jeshi hilo.


Alisema pamoja na changamoto ndogo zilizobaki, lakini anaamini serikali ijayo itazifanyia kazi na kuendeleza pale alipoishia ili kuwa na jeshi imara.

Tuesday, 20 October 2015

zikiwa zimebaki siku 5 kuelekea uchaguzi mkuu, huyu hapa kigogo mwingine wa ccm kutimkia ukawa

Dkt. Eve Sinare akihojiwa na Waandishi wa Habari

Wimbi la kujivua uanachama lazidi kuitafuna CCM, mwanachama mwingine muhimu aliyefanikisha mipango ya Ushindi wa Rais Jakaya Kikwete kuingia madarakani amehama CCM na kujiunga UKAWA.

Zikiwa zimebaki siku 5 kabla ya Oktoba 25, siku ambayo watanzania wataandika historia ya kuiweka madarakani serikali mpya ya awamu ya Tano, kada mwingine Mkongwe wa Chama hicho, ametangaza rasmi kujiweka kando.

Dkt. Eve Sinare, ambaye ni wakili wa kujitegemea aliyekuwa sehemu ya harakati za CCM,  alitangaza jana kukihama chama hicho akidai kuwa kimepoteza sifa za utawala bora na kimeshindwa kuwahudumiwa wananchi kwa kuwapa elimu bora iliyotarajiwa.

Dkt. Eve Sinare aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugeni ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA). Pia, ni Mwenyekiti Mtendaji wa Rex Attoneys na aliwahi kuteuliwa kuwa mmoja kati ya wajumbe wa Bodi ya Huduma ya Dunia iliyoko Texas inayofahamika kwa jina la World Services Group (WSG).

Hata hivyo, kama alivyosema Balozi Juma Mwapachu wakati anahama chama hicho, Dkt. Eve Sinare ameeleza kuwa hatajiunga na chama chochote cha siasa.

JK akumbushwa kutangaza mali alizochuma kabla ya kung'atuka.


Rais wa Tanzania
Mkurugenzi wa Idara ya Utetezi na Maboresho kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Harold Sungusia, amemkumbusha Rais Jakaya Kikwete, asiondoke kimyakimya bila kutangaza au kuorodhesha mali alizochuma wakati akiwa madarakani.

“Rais Kikwete alijaza fomu ya mali alizokuwa nazo Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, lakini hakutangaza. Tunasubiri kuona sasa baada ya kumaliza atatangaza mali aliyopata akiwa madarakani,” alisema.


Alisema mwaka 1995, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, alipoingia madarakani alitangaza mali zake, lakini alipong’atuka, ‘alisahau’ kutangaza, pengine ni kutokana na majukumu aliyokuwa nayo kitaifa sasa tunasubiri kuona kwa Rais Kikwete,” alisema.  


Kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13, 1995 na kanuni zake, mwananchi anaweza kupata taarifa za mali za viongozi kwa kufuata utaratibu uliopo, lakini baada ya kupata taarifa hizo, haruhusiwi kuzitangaza au kuzichapisha kwenye vyombo vya habari. 

Chanzo TUBONGE TZ

Chadema yamshtaki Kikwete UN.



Rais wa Tanzania
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema tayari kimeandika barua kwenda kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki Moon, kumshtaki Rais Jakaya Kikwete.

Mwanasheria wa Chadema, John Mallya, aliwaeleza waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuwa barua hiyo waliituma UN jana.


Mallya alisema lengo la barua ni kumshtaki Rais Kikwete kwa mataifa mengine kutokana na kauli yake ya kuwatisha Watanzania  aliyodai aliitoa Oktoba 14, mwaka huu ya kuwataka wapigakura kuondoka kituoni baada ya kupiga kura na endapo watakiuka watashughulikiwa.


Mallya alisema kauli ya Rais Kikwete ni kinyume cha Sheria ya Uchaguzi inayomtaka mpigakura kukaa mita 200 kutoka kituo cha kupigia kura.


“Kwa sababu Rais Kikwete hatuwezi kumshtaki kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, ziko mamlaka ambazo tunatumia kumshtaki kama tulivyofanya kuiandikia barua UN na kupeleka nakala Jumuiya ya Madola, Umoja wa Afrika, Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai na kusainiwa na Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Profesa Abdallah Safari,” alisema Mallya.


Chanzo... TUBONGE TZ

Daktari bandia awaambukiza Ukimwi watu 100


Mwanaume mmoja aliyejidai kuwa daktari na kuwaambukiza watu zaidi ya mia moja virusi amefikishwa mahakamani nchini Cambodia. Yamkini daktari huyo bandia alikuwa akiwadunga wagonjwa wake kwa sindano aliyokuwa ameitumia kwa mgonjwa aliyekuwa na virusi vya Ukimwi.

Yem Chhrin anakabiliwa na kosa la kuua na kuambukiza watu ugonjwa huo kwa kukusudia. Aidha Bw Yem anashtakiwa kwa kuwalaghai watu kuwa ni daktari ilhali hana vyeti halali vya kuhudumia umma. Iwapo atapatikana na hatia mahakama ya nchi hiyo huenda ikamhukumu kifungo cha maisha jela.

Waathiriwa walioambukizwa maradhi ya Ukimwi wanatokea katika kijiji cha Roka kilichoko Kaskazini Magharibi. Mmoja wao ni kiongozi wa kidini wa madhehebu ya Buddha na mtoto wa miaka mitatu.

Takriban 10 kati ya waathiriwa hao wanakisiwa kuwa wameshakata roho. Kwa mujibu wa ripoti za mahakama daktari huyo bandia amekiri kuhudumu bila vyeti maalum ila anakana kukusudia kuwaambukiza watu hao 100 virusi vinavyosababisha maradhi ya Ukimwi.

Monday, 19 October 2015

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA MRADI WA VITUO VYA MAPUMZIKO NA VYOO VYA WASAFIRI KATIKA BARABARA KUU NCHINI, KATIKA KIJIJI CHA IDETERO, MUFINDI-IRINGA.

 

   Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wananchi wa Kijiji cha Idetero Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa, wakati wa hafla ya uwekaji Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mradi wa Vituo vya Mapumziko na Vyoo vya Wasafiri katika Barabara Kuu nchini, juzi Okt 17, 2015.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mohamed Mgimwa, akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Makamu wa Rais Dkt. Bilal, kuhutubia wananchi wa Kijiji cha Idetero Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa, wakati wa hafla ya uwekaji Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mradi wa Vituo vya Mapumziko na Vyoo vya Wasafiri katika Barabara Kuu nchini, juzi Okt 17, 2015.
 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifunua kitambaa kuweka Jiwe la Msingi la wa Mradi wa Vituo vya Mapumziko na Vyoo vya Wasafiri katika Barabara Kuu nchini, wakati wa hafla ya kuweka jiwe la Msingi iliyofanyika katika Kijiji cha Idetero Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa juzi Okt. 17, 2015.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo ya ujenzi huo kutoka kwa msimamizi wa Ujenzi, Stanley Ndosite Nzowa, wakati wa hafla ya uwekaji Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mradi wa Vituo vya Mapumziko na Vyoo vya Wasafiri katika Barabara Kuu nchini, juzi Okt 17, 2015.

Tuesday, 22 September 2015

Walinzi wa rais Burkina Faso ‘kupigana’

Burkina Demos
Wanajeshi wamelakiwa kwa shangwe na waandamanaji ambao wamekuwa wakipinga mapinduzi
Viongozi wa mapinduzi Burkina Faso wamekataa kutii makataa ya kusalimu amri na kutishia kupigana vita wakishambuliwa.

Walinzi wa rais walioongoza mapinduzi walikuwa wamepewa hadi saa nne saa za huko kuweka chini silaha na wanajeshi ambao walifika katika mji mkuu Ouagadougou usiku.

 

Hayo yamejiri huku marais wa mataifa ya Afrika Magharibi chini ya muungano wa Ecowas wakikusanyika Abuja, Nigeria kufahamishwa na Rais wa Senegal Macky Sall kuhusu hatua zilizopigwa katika kutatua mzozo huo.

Duru zinasema mashaurino ya kupatanisha wanajeshi hao na walinzi waliopindua serikali yaligonga mwamba usiku, suala tata likiwa hatima ya walinzi hao wa rais.

Rais Sall amekuwa akiongoza mashauriano akishirikiana na mwenzake wa Benin Yayi Boni.
Barabara za kuelekea ikulu ya rais hazina watu wala magari huku hali ya wasiwasi ikiendelea kutanda Ouagadougou.

Kiongozi wa mapinduzi Jenerali Gilbert Diendere alikuwa awali ameambia BBC kwamba yuko tayari kurejesha mamlaka kwa uongozi wa kiraia, lakini baada tu ya mpango wake wa kumaliza mzozo wa sasa kuungwa mkono na viongozi wa mataifa ya eneo hilo.

Akiongea kutoka mafichoni, Jenerali Diendere aliambia BBC: “Kuwa tayari kusalimu amri? Hatujafika huko bado …Tungependa kuendelea na mazungumzo na tunawaambia wote kwamba tuko tayari kutekeleza maamuzi ya Ecowas (kundi la mataifa ya Afrika Magharibi).”

Aidha, aliomba radhi kwa raia, akisema hilo tu ndilo wawezalo kufanya kwa sasa.

Walinzi wa rais waliopindua serikali ni watiifu kwa kiongozi aliyetimuliwa mamlakani mwaka jana Blaise Compaore.

Walimzuilia Kaimu Rais Michel Kafando Jumatano iliyopita, na kumtangaza Jenerali Diendere kuwa kiongozi mpya.

Tangu wakati huo, watu 10 wameuawa kwenye makabiliano kati ya waandamanaji wanaopinga mapinduzi hayo na maafisa wa usalama. Watu zaidi ya 100 wamejeruhiwa.

Balozi wa Ufaransa nchini Burkina Faso, Gilles Thibault, aliandika kwenye Twitter kwamba Bw Kafando ameachiliwa huru na sasa yumo kwenye makao ya balozi huyo.

Monday, 21 September 2015

MWALIMU ALIYETOWEKA MABAKI YA MWILI WAKE YAPATIKANA SHAMBANI KWA MWALIMU MWENZAKE....

 

 Mabaki ya Mwili wa Aliyekuwa Mwalimi mkuu shule ya msingi Muholo kata ya Luana wilayani Ludewa katika Mkoa wa Njombe aliyepotea ktk mazingira ya kutatanisha tareh 29 mei 2015 Majuto Haule mwili wake umekutwa umefukiwa katika shamba la mwalimu Vincent Haule Nje kidogo ya kijiji cha Muholo leo

Wednesday, 16 September 2015

wazazi wa luke shaw wamshuhudia mtoto wao akiumia uwanjani>> na kusema hivi

 2C5A626400000578-0-image-a-17_1442391403899

Kumbe jana usiku wakati Luke Shaw anapata jeraha kubwa ambalo litamfanya akae nje ya uwanja angalau kwa miezi 6, wazazi wake walikuwepo uwanjani kumuangalia mtoto wao akicheza mechi ile.

Bahati mbaya wamemshuhudia mtoto wao akipata maumivu makali badala ya kumuona akiisaidia club yake. Taarifa zinasema kwamba wazazi hao walishindwa kumalizia kuangalia mechi walielekea hospitali ambapo Luke alipelekwa. Siku ya leo Luke Shaw anategemea kufanyiwa matibabu kamili ili kuendelea kuuguza mguu wake.

Luke amelazwa kwenye hospitali ya St Anna Ziekenhuis ambapo Ed Woodward amemtembelea leo asubuhi.

Moreno ambae alihusikka kwenye rafu hiyo alisema, “Najiskia vibaya sana kwake najiskia vibaya snaa kwasababu najua jinsi anavyojiskia. Kitu kama kile kimewai kunitokea mimi kwenye kombe la dunia. Namtakia heri apone haraka na halikua lengo langu”

RATIBA YA MECH ZA LEO UEFA Champions League

UEFA Champions League




Bayer Levkn v BATE Bor 21:45 at BayArena
Roma v Barcelona 21:45 at Olimpico
Dinamo Zagreb v Arsenal 21:45 at Maksimir

Olympiakos v Bayern Mun 21:45 at Georgios Karaiskakis Stadium

Chelsea v Maccabi Tel Aviv 21:45 at Stamford Bridge

Dynamo Kiev v FC Porto 21:45 at Kiev Olympic Stadium

KAA Gent v Lyon 21:45 at Ghelamco Arena

Valencia v Zenit St P 21:45 at Mestalla

Wagombea wa michezo ya Olimpiki 2024 watangazwa

 

Wanaogombea kuandaa mashindano ya michezo ya Olimpiki mnamo mwaka 2024 wametangazwa.
Miji hiyo ni pamoja na Paris- Ufaransa, Roma- Italia, Los Angeles nchini Marekani, Budapest pamoja na Hamburg.

Maamuzi ya mwisho yatatangazwa nchini Peru katika mkutano wa kamati kuu ya Olimpiki katika kipindi cha miaka miwili ijayo.

Mwaandishi wa habari za michezo wa BBC , anasema kuwa miji miwili ambayo inapigiwa upatu wa kuteuliwa ni Paris na Los Angeles.

Bondia afariki baada ya kupigwa 'knock out'

David Browne
Mwana masumbwi mmoja wa Australia amefariki siku nne baada ya kupoteza fahamu alipopigwa 'knock out' katika pigano la kijimbo mjini Sidney.

Davey Browne mwenye umri wa miaka 28 aliangushwa na Carlo Magali wa taifa la Ufilipino mwisho wa raundi ya 12 katika taji la uzani wa Feather siku ya Ijumaa.

Brown ambaye ni baba ya watoto wawili alipelekwa katika chumba cha wagonjwa mahututi kabla ya mitambo inayomsadia kuzimwa alipokosa kuimarika kiafya.

Muungano wa wahudumu wa matibabu nchini Australia umetaka mchezo wa ndondi kupigwa marufuku nchini humo kufuatia kifo hicho.

Kifo cha Browne kinajiri wiki sita baada ya mwanamasumbwi wa Queensland Braydon Smith kuzirai na kufariki kufuatia pigano la uzani wa Feather nyumbani kwake huko Toowoomba.

Hapatoshi >>>Lissu amjibu JK, Kuhusiana na SAKATA LA Richmond

Pg 1 lowassa

MWANASHERIA mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, amemkingia kifua mgombea urais wa chama hicho, Edward Lowassa akisema hahusiki na sakata la Richmond.

Lissu ametoa kauli hiyo siku moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kunukuliwa na gazeti moja akisema kuwa muhusika wa Richmond ni yule anayetembea na Lissu katika kampeni huku akimtaka amtaje kabla Rais Kikwete hajafanya hivyo.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika Viwanja  vya Shule  ya Msingi  ya Kiwanja  cha  Ndege Manispaa  ya Morogoro jana, Lissu alimtaja kwa jina kigogo wa serikali akisema ndiye muhusika mkuu wa  wa Richmond na si Lowassa.

Kauli hiyo ya Lissu haitofautiani na ile ya Lowassa aliyoitoa alipokuwa akijiunga na Chadema ambapo alisema katika moja ya vikao vya serikali vya kujadili sakata hilo, kiongozi mmoja alisema amepata amri kutoka ngazi za juu kwamba asaini mkataba wa kampuni hiyo.

Lissu alisema ni vema Watanzania kutambua kuwa mmiliki halali wa Richmond ambayo imebadilishwa majina kutoka Dowans hadi Symbion kwa sasa yupo ngazi za juu serikalini.
‘’Huyu mzee wa watu wameshampaka matope vya kutosha na wala hajatoka mbele za watu kulalamika, anatumia busara zaidi.

‘’Tunaishangaa serikali kuendelea kuwadanganya wananchi bila ya huruma kwa kudai kampuni hizo zote zinamilikiwa na Lowassa, kama  kungekuwa na ukweli wowote, kwanini wanaendelea  kulipa hayo madeni  ya mabilioni ya fedha?

“Ni lazima Watanzania watambue kuwa Richmond ilijadiliwa bungeni ikiwa chini ya mwenyekiti wake Dk. Harisson Mwakyembe  ambaye alikuwa kwenye kamati ya Bunge iliyochunguza mkataba wa Kampuni ya Richmond na mwishowe kuja kuibuka kashfa ya mafisadi  ambao walikuwa 11,” alisema na kuongeza.

“Katika mlolongo wa mafisadi waliotajwa namba tisa alitajwa Lowassa wakati akiwa waziri mkuu, lakini hakuhusika moja moja na suala hilo,” alisema.

Lissu alisema katika orodha hiyo namba 10 alitajwa kiongozi mmoja mstaafu na baadae akataja tena jina la kigogo mwingine ambaye alisema huyo ndiye mmiliki wa kampuni hiyo.
Alisema Lowassa ambaye anatembea naye katika kampeni zake hahusiki hata kidogo na suala hilo ila aliwajibika kisiasa ili kuiokoa serikali, kwa kuwa alikuwa msimamizi wa serikali hiyo.
Lissu alisema ili kuondoa mfumo mbovu ni lazima wahakikishe wanaing’oa serikali iliyopo madarakani kwa kipindi cha muda mrefu, kwani hiyo ndio chanzo kikuu cha umaskini.

Lowassa: na wakulima
Kwa upande wake Lowassa, alisema serikali yake itakuwa rafiki kwa wakulima na wafugaji na kuwa atatoa elimu bora bila malipo yoyote.

“Hakutakuwa na mambo ya michango ya ajabu ajabu, tutatoa elimu ya bure lakini iliyo bora,” alisema.
Kuhusu suala la viwanda vya miwa, alisema atahakikisha viwanda vinavyowezekana vitarudishwa mikononi mwa serikali.
Alisema pia kuwa, wafanyabiashara ndogo ndogo wakiwamo mama lishe na bodaboda, atawahakikisha wanaendelea kuwa rafiki zake.

Sumaye: CCM inahukumiwa kwa uongo wake
 Waziri  mkuu  mstaafu, Fredrick Sumaye,  alisema   kwa sasa CCM   inahukumiwa  kwa  kusema  uongo  kwa  kipindi cha  miaka 50 tangu  taifa lipate  uhuru 

Alisema katika kipindi hicho, chama hicho kimeshindwa kukidhi mahitaji muhimu ya Watanzania, hivyo wananchi wamechoka  kudanganywa .

Aidha Sumaye  alidai  Watanzania  bado  wamekuwa  wakiishi  katika mazingira  magumu  na  yenye  shida  pamoja  na CCM  kuja  na  sera  yake  ya  uongo  ya maisha  bora  kwa kila Mtanzania .
“Ni wazi  hakuna  ubishi  kama  Watanzania  sasa  wamechoshwa  na uongo wa CCM, ndio  maana   wametuunga  mkono  kwa  asilimia 100  katika mikutano  yote  ya  Ukawa  pasipo  kuletwa  na magari  kama  ilivyo  katika mikutano  yao”alisema  Sumaye .

Alisema uongo  wa CCM unajionesha  wazi wazi  kwenye  sekta  ya  kilimo, afya , miundombinu, elimu  na  kudai   kuwa  hayo  ni maeneo ambayo  yanawatesa  kwa  kiasi  kikubwa na kuyaona maisha  kuwa  magumu.

Alisema  kuwa  dalili  za  Watanzania  kuunga mkono  ukawa  ni  dalili  tosha  kuonesha  wanahitaji mabadiliko  ndani  ya   taifa , pasipo  kushawishika  na pesa .

“Hapa  mmekuja  kwa  upendo  wenu na taifa lenu hamjaletwa  kwa  magari  kama  ilivyo  katika  mikutano  yao (CCM),” aliongeza  Sumaye .

Naye Mjumbe  wa Kamati  ya Utendaji  Kanda  ya  Kati wa Chadema, Mathew Likwina  akizungumza na  wanachama  wa  chama  hicho alisema  kuwa  lengo  la UKAWA   ni  kufanya  mabadiliko   ya  kimfumo.

Alisema  kuwa  kuondoa  mfumo sio  kubadilisha  kiongozi  mmoja  wa ccm  , bali  ni kuondoa  uongozi  wote  wa  CCM usio  na mfumo mzuri  katika  kuleta maendeleo  ya  taifa  na watu  wake .
Aidha   alidai  kuwa  kama  Watanzania  wataiondoa CCM  taifa  linauhakika  mkubwa   wa  kuwa na mfumo mzuri Wenye  kujali   maslahi  ya wananchi badala  ya  sasa  CCM imekuwa na mifumo  ya  kujali  watu wachache  na  familia  zao .

NEC: Lushoto hawatapiga kura ya ubunge

JAJILUBUVA

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imesema wananchi wa Jimbo la Lushoto mkoani Tanga, hawatapiga kura ya kuchagua mbunge katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25.

Hatua hiyo, inatokana na kufariki dunia kwa aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa mwamvuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Mohamed Mtoi (39).

Mtoi, alifariki dunia Jumamosi iliyopita baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kuacha njia na kupinduka kisha kudumbukia kwenye korongo wilayani Lushoto.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva, alisema sheria inaruhusu kama mgombea atafariki dunia wakati huu wa uchaguzi uahirishwe.

“Wananchi wa Lushoto hawatapiga kura ya mbunge Oktoba 25, tumeahirisha hadi hapo baadaye tutakapowatangazia na chama husika kitapokuwa kimepata mgombea,” alisema Jaji Lubuva.

Kulingana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Zubery Mwombeji, Mtoi alipata ajali katika eneo la Magamba Coast, Kata ya Magamba wilayani Lushoto.

Alisema gari hilo lilikuwa likiendeshwa na Miraj Nuru (43), likitokea Tarafa ya Mlola kwenda Mkuzi baada ya kumaliza shughuli za kampeni.

Facebook, Kuja na mabadiliko haya wakati wowote !!



 

Facebook ndio mtandao wa Kijamii ambao unatumiwa na watu wengi zaidi, Takwimu zinaonesha Duniani kuna jumla ya watu kama Bilioni 7 hivi, alafu Ripoti ya The Statistics Portal 2015 inaonesha watumiaji wa Mitandao ya Kijamii wako Bilioni 1.96, na kati yao zaidi ya 70% ni watumiaji wa mtandao wa Facebook !!

3d illustration of a facebook logo standing in front of an upright map of the world on a blue reflective surface

Mark Zuckerberg katupasha kuhusu mipango mingine ya Facebook, sasahivi kama ukiandika post yoyote au ukiingia kwenye ukurasa wa mtu yoyote wa Facebook unakutana na alama tatu, alama ya ‘LIKE’, ‘COMMENT’ na alama ya ‘SHARE’… lakini  CEO Zackerberg anasema ni maombi ya muda mrefu watumiaji wa Facebook wanataka iwepo na alama ya DISLIKE, yani kama kitu hujakipenda unabonyeza tu hapo. 

 1014_mark-zuckerberg-e1413303739290-1940x1091
Watu wengi wameulizia kuhusu kuwepo alama hiyo, leo ni siku maalum kwa sababu natangaza rasmi kwamba tunashughulikia hicho kitu na muda sio mrefu tutakiweka kwenye majaribio‘ >>> Mark Zuckerberg.

UEFA: Man United, Man City zachapwa


Timu za Uingereza za Man United na Man City zimeanza vibaya michuano ya kombe la kilabu bingwa barani Ulaya baada ya kuchapwa.

Man United wakiwa ugenini nchini Uholanzi wamelala kwa kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya PSV. Memphis Depay alianza kuifungia timu yake bao la kwanza kabla ya Héctor Moreno wa PSV kusawazisha kisha Luciano Narsingh akafunga bao la ushindi.

Man City nao wakiwa katika dimba lao la Etihad walikubali kipigo cha mabao 2-1 toka kwa vibibi vizee vya Turin Juventus mabao ya Juve yakifungwa na Álvaro Morata na Mario Mandzukic huku bao la kujifunga la beki Giorgio Chiellini, likiwapa Man City bao moja.

Real Madrid wakiwa nyumbani Santiago Bernabeu wameshinda kwa kishindo kwa ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Shakhtar Donetsk, Cristiano Ronaldo akifunga hat trick na Karim Benzema akifunga bao moja.

Matokeo mengine ya michuano hii ni:
PSG 2 – 0 Malmö FF
VfL Wolfsburg 1 – 0 CSKA
Benfica 2 – 0 FC Astana
Galatasaray 0 – 2 Atletico Madrid
Sevilla 3 – 0 Borussia Mönchengladbach

Monday, 14 September 2015

Jeshi la Misri ladai kuua watu 12 kimakosa

Kikosi maalum kimetumwa kuchunguza tukio la mauaji

Misri imesema jeshi lake la ulinzi limeua raia 12 kwa bahati mbaya,wakiwemo watalii kutoka Mexico wakati wa operesheni ya kupambana na ugaidi.

Wizara ya mambo ya ndani ya nchi hiyo imetuma kikosi kwa ajili ya kufanya uchunguzi kuhusu tukio hilo

kwa upande wa Rais wa Mexico, Enrique Pena Nieto amekemea tukio hilo na kusema kuwa ameitaka serikali ya Misri kufanya uchunguzi wa kina, Wizara ya mambo ya nje ya Mexico imethibitisha kuwa takriban raia wake wawili wameuawa na kuongeza kuwa inafanya jitihada kuwatambua waathirika wengine.

tamko la wizara limesema , Balozi wa Mexico nchini Misri, Jorge Alvarez Fuentes alitembelea hospitali na kuzungumza na raia watano wa Mexico ambao hali zao zilikuwa njema.

Saturday, 12 September 2015

Serena William apata pigo kwenye mchezo wake wa Nusu fainali



Serena katika mkutano na vyombo vya habari baada ya mechi hiyo.


Bingwa wa mchezo wa tenisi upande wa wanawake Serena Williams amepata pigo kubwa katika mashindano ya US Open baada ya kushindwa kwa seti 2-6 6-4 6-4 na Muitaliano Roberta Vinci katika nusu fainali.

''Ni pigo kubwa'', alisema aliyekuwa bingwa mara mbili katika mchezo huo Tracy Austin.
''Hili ni pigo kubwa katika historia ya mchezo huu kutokana na kile kilichofanyika''.


Serena akisalimiana na Vinci baada ya mechi hiyo



William alianza mechi hiyo akiwa hajashindwa katika mechi 33 katika Grand Slum tangu machindano ya Wimbledon ya mwaka 2014.

Alikuwa amejitahidi kufikia rekodi iliowekwa na Steffi Graf ya mwaka 1988 ambapo mwana dada huyo alizoa mataji yote mwaka huo na alikuwa akikabiliana na mchezaji ambaye alimshinda mara nne bila kushindwa seti moja.


Thursday, 2 July 2015

Ugiriki yaonywa kuhusu kura ya 'La'


Raia wa Ugiriki
Raia wamegawanyika huku wengi wakianza kuhamia kambi ya 'Ndio'

Ugiriki imeonywa dhidi ya kupiga kura ya 'La' wakati wa kura ya maoni hapo Jumapili kwa sababu haitasaidia kutatua matatizo ya kiuchumi yanayokumba taifa hilo.

Hofu ya Ebola DRC



Mgonjwa wa Ebola DRC 
Watu wanne wamefariki dunia wakiwa na dalili za ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Boko Haram yashambulia zaidi

Boko haram wazidisha mashambulizi
Watu 150 wameuawa baada ya Boko Haram kuvamia kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Walioshuhudia mashambulizi hayo wanasema watu tisini na saba wameuawa siku ya Jumatano katika kijiji cha Kukawa kilichopo karibu na Ziwa Chad.

Habari zinasema pia wanaume 48 wamepigwa risasi na wapiganaji katika mashambulizi tofauti siku ya Jumanne.

Mashuhuda wanaokimbia eneo lililopo karibu na Ziwa Chad wanasema idadi kubwa ya wapiganaji wamevamia vijiji vitatu ambapo wameuwa wanaume, wanawake na watoto.

Baadhi ya ripoti zinasema walipigwa risasi huku wengine wakielezea jinsi wapiganaji hao walivyowachinja watu na kuchoma majengo.

Upande wa Kusini, nje kidogo na mji wa Monguno, kundi la wapiganaji wa Boko Haram wamefika usiku wakati watu walipokuwa wanaswali. Waliwasubiri mpaka walipomaliza kuswali na kuwatenganisha wanaume na wanawake na baadae kuanza kuwamiminia risasi wanaume.

Mwanasiasa anayewakilisha eneo hilo, Mohammed Tahir amesema awali alitoa tahadhari kwa jeshi la Nigeria kwamba vijiji hivyo viko hatarini kwa sababu Boko Haram wameweka makazi katika maeneo hayo baada ya kutimuliwa katika himaya yao ya msitu wa Sambisa. 

Haya ni mashambulizi mabaya zaidi kufanywa na Boko Haram katika kipindi cha wiki kadhaa.
Kundi hilo limekuwa likilipuwa mabomu kadhaa baada ya kudhoofishwa na majeshi ya Nigeria.

Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari amesema kipaumbele chake ni kuimarisha mapambano dhidi ya Boko Haram.

Msumbiji yakubali mapenzi ya jinsia moja

Wapenzi wa Jinsia moja
Nchi chache Afrika zimekubali mapenzi ya jinsia moja
Msumbiji imehalalisha mapenzi ya jinsia moja,na kuwa moja wapo wa nchi chache Afrika zinazohalalisha mapenzi ya jinsia moja.

Sheria hiyo iliyowekwa na wakoloni wa nchi hiyo Ureno iliondolewa na bunge la nchi.Watetezi wa haki za wapenzi wa jinsia moja,wametaja hatua hiyo kama ushindi mkubwa.

Hata hivyo nchi nyingi za Afrika zimeweka sheria kali dhidi ya mapenzi ya jinsia moja.Nigeria ilipiga marufuku na kuweka adhabu ya kifungo cha miaka 14 jela kwa wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.Uganda nayo imeapa kurejesha sheria kali kuharamisha mapenzi ya jinsia moja.

Sheria ya awali ilitupiliwa nje na mahakama ya kikatiba.

Msumbiji sasa anajiunga na mataifa mengine ikiwa ni pamoja na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Ivory Coast na Afrika Kusini ambapo siyo hatia kuwa mpenzi wa jinsia moja.

Vikwazo kwa makamanda wa S Sudan


Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limewawekea vikwazo ikiwemo marufuku ya usafiri na kupiga tanji mali za majenerali sita wa Sudan Kusini.
Watatu ni kutoka upande wa serikali na wengine watatu ni kutoka upande wa waasi.
Wapiganaji Sudan Kusini
Watoto wengi wamelazimishwa kuwa wapiganaji Sudan Kusini

BREAKING NEWS-Bunge Laharishwa gafla baada ya Wabunge wa UKAWA kugomea Miswada Petroli na Gesi

 
wanachokiita wanaburuzwa, Wabunge wa UKAWA kwa pamoja wamegoma kuendelea na bunge na wote kuamua kusimama baada ya kupinga uwasilishaji wa dharula wa Miswada mitatu muhimu ya Gesi, Petroli na Uziduaji "Extractive Industries". 

Ni baada ya John Mnyika kuomba Muongozo juu ya uvunjaji wa kanuni za bunge. shuguli za leo zimekiuka kanuni kwani miswada imewekwa ikiwa sambamba. anasema hoja ikishatolewa ni lazima ijadiliwe iamuliwe ndo itolewe hoja nyingine, lakini leo zipo hoja tatu kwa pamoja.



Mnyika kasema na huu Muongozo sitaki useme utautolea ufafanuzi siku nyingine kwa maana hatuwezi kuendelea kufanya kazi ambazo zimevunja kanuni.

Wanapinga kuwasilishwa kwa dharula na kwa pamoja Miswada yenye manufaa makubwa kwa nchi.

Miswada wanayo pinga na iliyo wasilishwa kwa pamoja ni;

1.Muswada juu ya Petroli, 2015 (The Petroleum Act, 2015):

2.Muswada juu ya Usimamizi wa Mafuta na Gesi, 2015 (The Oil and Gas Revenues Management Act, 2015):

3.Muswada juu ya tasnia ya Uziduaji Tanzania (The Tanzania Extractive Industries Act, 2015): The Tanzania Extractive Industries Act, 2015.

Hata baada ya Spika kuwataka watoke nje kama hawataki kuendelea, Wamegoma na kusimama na kuanza kupiga kelele hadi Spika akaahirisha bunge. UKAWA wamesema mwanaharamu hapiti leo
.

Chadema yaibwaga CCM mahakamani

Chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara imezidi kupata pigo baada ya Mahakama kutengua matokeo ya uchaguzi wa wenyeviti wa vitongoji 16 vya mji mdogo wa Mirerani, kwa maelezo kuwa ulikiuka sheria na utaratibu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Hii ni mara ya pili katika kipindi cha mwezi mmoja kwa Mahakama kutengua matokeo ya uchaguzi huo ambao uliwaweka madarakani makada wa CCM.

Awali, Mei 30 Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Kiteto ilitengua matokeo ya uchaguzi wa mwenyekiti wa Kijiji cha Lobosireti kwa kukiuka sheria na utaratibu.

Chadema ilifungua kesi kadhaa mahakamani hapo kupinga kitendo cha wagombea wa CCM kupewa ushindi bila kufanya uchaguzi Desemba 14, mwaka jana.

Hukumu hiyo ya jana, inatokana na kesi zilizofunguliwa na Chadema wilayani Simanjiro kwenye kata za Endiamtu na Mirerani, wakipinga wagombea wa CCM kupewa ushindi bila kupigiwa kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Desemba 14 mwaka jana.

Hakimu Mkazi Mfawidhi mahakama hiyo, Elimo Massawe aliagiza kurudiwa kwa uchaguzi wa viongozi wa vitongoji vya Zaire, Kisimani, Tenki la Maji, Endiamtu, Kairo na Kazamoyo vilivyoko Kata ya Ediamtu.

Hakimu Massawe alitaja vitongoji vingine kuwa ni Sekondari, Kilimahewa, Tanesco, Kazamoyo Juu, Mji mpya, Tupendane na vitongoji vya Kata ya Mirerani ambavyo ni Kangaroo, Songambele A, Getini na Songambele B.

Katika kesi hiyo, Chadema iliwakilishwa na mawakili James Millya, Shadrack Kimomogoro na Daudi Haraka na Mahakama iliamuru walipwe Sh160 milioni za gharama za kesi hiyo ambayo ilichukua takribani miezi sita hadi kutolewa hukumu.

Katibu Mwenezi wa Chadema mkoani Manyara, Ambrose Ndege alisema Mahakama imetenda haki kwa kutoa hukumu sahihi na wanajipanga ipasavyo kuhakikisha watashinda vitongoji vyote pindi uchaguzi huo utakaporudiwa.

“Tuliwaeleza tangu awali kuwa uchaguzi ukifanyika tutawashinda saa nne asubuhi hivyo tunawasubiri uwanjani na tutaongoza Mamlaka ya Mji wa Mirerani kwani wananchi wanatukubali,” alisema Ndege.

Hata hivyo, Katibu Mwenezi wa CCM wa Kata ya Endiamtu, Mashaka Jeroro alisema wanatarajia kukata rufaa kupinga hukumu hiyo akisema wagombea wa Chadema walikosea kujaza fomu ndiyo sababu wakawekewa pingamizi.

Upinzani wambana Dk Migiro, AG bungeni


Waziri Kivuli wa Sheria (Chadema), Tundu Lissu akichangia  muswada wa Kuwalinda Watoa Taarifa za Uhalifu na Mashahidi wa mwaka 2015 bungeni mjini Dodoma jana. 
Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Asha Rose Migiro, jana alibanwa bungeni baada ya wabunge wa upinzani kuhoji juu ya Muswada wa Sheria ya Kulinda Watoa Taarifa za Uhalifu na Mashahidi wa mwaka 2015 wakieleza umewahishwa bila sababu yoyote.

Dk Migiro alikutana na kimbuga cha upinzani ikiwa ni siku moja baada ya Bunge la 10 kuigomea Serikali ilipotaka kuingiza bungeni miswada mitatu iliyohusu Wizara ya Nishati na Madini wakisema inahitaji muda mzuri.

Mapema jana, Dk Migiro aliwasilisha ndani ya Bunge muswada huo akilitaka lijadili na kuupitisha ili kutoa nafasi ya kuwalinda watu wa aina hiyo.

Akiwasilisha maoni ya upinzani bungeni, msemaji wa kambi hiyo katika Wizara ya Katiba na Sheria, Tundu Lissu alisema muswada huo hauna tija kwa muda huo kwani unatoa nafasi finyu kwa wabunge kujadili jambo ambalo ni muhimu zaidi kwa wananchi.

Lissu ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), alisema uharaka wa muswada huo ni kiashiria tosha kwamba Serikali inataka kuminya uhuru wa wabunge kupitia kwa kina sheria hiyo.

“Kanuni zinasema kuwa, sheria inaweza kupitishwa kwa hati ya dharura ikiwa tu kuna mambo ambayo yanataka kutokea ambayo ni pamoja na majanga au vita. Je, kuna uharaka kiasi gani wa kupitisha muswada huu?” alihoji Lissu.

Mbunge huyo mbali na kutoa ufafanuzi katika vifungu vingi katika muswada huo, lakini alisisitiza kuwa ukipitishwa utakuwa umewanyima haki watu wa kada ya chini na kuwapa mwanya viongozi wao.

Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika alipinga vikali muswada huo pamoja na namna ulivyowasilishwa na akazua mgogoro mkubwa baina yake na Mwanasheria Mkuu wa Serikali(AG), George Masaju.

Malumbano ya wawili hao yalianzia pale Mnyika aliposema kuwa Serikali ni dhaifu katika suala zima la utungaji wa sheria jambo ambalo pia liliamsha hasira za Spika. 
Katika hoja zake, Mnyika alipinga jinsi muswada ulivyokuwa ukitoa upenyo kwa watu kutoa taarifa kwa wakubwa wao badala ya kuzipeleka kwa vyombo vingine.

“Mfano, muswada unaelekeza mtu kutoa taarifa kwa kiongozi wake yaani akiwa mfanyakazi wa benki kuu anawezaje kutoa taarifa za ufisadi wa gavana kwa gavana mwenyewe?” alihoji Mnyika.

AG Masaju alipinga kauli za kuwa Serikali inafanya vitu dhaifu akisema siyo nia yao, bali wanafanya kazi ya kupeleka miswada ili wabunge wenyewe ndiyo wafanye uamuzi.