This is default featured post 1 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured post 2 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured post 3 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured post 4 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured post 5 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
Tuesday, 27 October 2015
MBATIA AMLAZA CHALI MZEE ELYIATONGA MREMA JIMBO LA VUNJO
MAWAZIRI WA JK WLIOANGUKA KWENYE NAFASI YA UBUNGE MWAKA HUU 2015

Wednesday, 21 October 2015
mkuu wa majeshi ya ulinzi nchini Jenerali davis mwamunyange aonekana
![]() |
| Jenerali Davis Mwamunyange |
Alisema hakuna nchi inayoweza kupata maendeleo mbalimbali kama haina jeshi imara kutokana na kuwapo vitendea kazi vya kutosha na madhubuti vinavyoimarisha jeshi hilo.
Jenerali Mwamunyange alisema katika kipindi chote cha uongozi wa Rais Kikwete, ameimarisha JWTZ na kutimiza mahitaji ya jeshi hilo.
Alisema pamoja na changamoto ndogo zilizobaki, lakini anaamini serikali ijayo itazifanyia kazi na kuendeleza pale alipoishia ili kuwa na jeshi imara.
Tuesday, 20 October 2015
zikiwa zimebaki siku 5 kuelekea uchaguzi mkuu, huyu hapa kigogo mwingine wa ccm kutimkia ukawa
![]() |
| Dkt. Eve Sinare akihojiwa na Waandishi wa Habari |
Wimbi la kujivua uanachama lazidi kuitafuna CCM, mwanachama mwingine muhimu aliyefanikisha mipango ya Ushindi wa Rais Jakaya Kikwete kuingia madarakani amehama CCM na kujiunga UKAWA.
Zikiwa zimebaki siku 5 kabla ya Oktoba 25, siku ambayo watanzania wataandika historia ya kuiweka madarakani serikali mpya ya awamu ya Tano, kada mwingine Mkongwe wa Chama hicho, ametangaza rasmi kujiweka kando.
JK akumbushwa kutangaza mali alizochuma kabla ya kung'atuka.
![]() |
| Rais wa Tanzania |
“Rais Kikwete alijaza fomu ya mali alizokuwa nazo Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, lakini hakutangaza. Tunasubiri kuona sasa baada ya kumaliza atatangaza mali aliyopata akiwa madarakani,” alisema.
Alisema mwaka 1995, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, alipoingia madarakani alitangaza mali zake, lakini alipong’atuka, ‘alisahau’ kutangaza, pengine ni kutokana na majukumu aliyokuwa nayo kitaifa sasa tunasubiri kuona kwa Rais Kikwete,” alisema.
Kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13, 1995 na kanuni zake, mwananchi anaweza kupata taarifa za mali za viongozi kwa kufuata utaratibu uliopo, lakini baada ya kupata taarifa hizo, haruhusiwi kuzitangaza au kuzichapisha kwenye vyombo vya habari.
Chanzo TUBONGE TZ
Chadema yamshtaki Kikwete UN.
![]() |
| Rais wa Tanzania |
Mwanasheria wa Chadema, John Mallya, aliwaeleza waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuwa barua hiyo waliituma UN jana.
Mallya alisema lengo la barua ni kumshtaki Rais Kikwete kwa mataifa mengine kutokana na kauli yake ya kuwatisha Watanzania aliyodai aliitoa Oktoba 14, mwaka huu ya kuwataka wapigakura kuondoka kituoni baada ya kupiga kura na endapo watakiuka watashughulikiwa.
Mallya alisema kauli ya Rais Kikwete ni kinyume cha Sheria ya Uchaguzi inayomtaka mpigakura kukaa mita 200 kutoka kituo cha kupigia kura.
“Kwa sababu Rais Kikwete hatuwezi kumshtaki kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, ziko mamlaka ambazo tunatumia kumshtaki kama tulivyofanya kuiandikia barua UN na kupeleka nakala Jumuiya ya Madola, Umoja wa Afrika, Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai na kusainiwa na Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Profesa Abdallah Safari,” alisema Mallya.
Chanzo... TUBONGE TZ
Daktari bandia awaambukiza Ukimwi watu 100
Mwanaume mmoja aliyejidai kuwa daktari na kuwaambukiza watu zaidi ya mia moja virusi amefikishwa mahakamani nchini Cambodia. Yamkini daktari huyo bandia alikuwa akiwadunga wagonjwa wake kwa sindano aliyokuwa ameitumia kwa mgonjwa aliyekuwa na virusi vya Ukimwi.
Yem Chhrin anakabiliwa na kosa la kuua na kuambukiza watu ugonjwa huo kwa kukusudia. Aidha Bw Yem anashtakiwa kwa kuwalaghai watu kuwa ni daktari ilhali hana vyeti halali vya kuhudumia umma. Iwapo atapatikana na hatia mahakama ya nchi hiyo huenda ikamhukumu kifungo cha maisha jela.
Waathiriwa walioambukizwa maradhi ya Ukimwi wanatokea katika kijiji cha Roka kilichoko Kaskazini Magharibi. Mmoja wao ni kiongozi wa kidini wa madhehebu ya Buddha na mtoto wa miaka mitatu.
Takriban 10 kati ya waathiriwa hao wanakisiwa kuwa wameshakata roho. Kwa mujibu wa ripoti za mahakama daktari huyo bandia amekiri kuhudumu bila vyeti maalum ila anakana kukusudia kuwaambukiza watu hao 100 virusi vinavyosababisha maradhi ya Ukimwi.
Monday, 19 October 2015
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA MRADI WA VITUO VYA MAPUMZIKO NA VYOO VYA WASAFIRI KATIKA BARABARA KUU NCHINI, KATIKA KIJIJI CHA IDETERO, MUFINDI-IRINGA.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akihutubia wananchi wa Kijiji cha Idetero Wilaya ya Mufindi Mkoa wa
Iringa, wakati wa hafla ya uwekaji Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mradi wa
Vituo vya Mapumziko na Vyoo vya Wasafiri katika Barabara Kuu nchini, juzi
Okt 17, 2015.
Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mohamed Mgimwa, akizungumza kabla ya
kumkaribisha mgeni rasmi Makamu wa Rais Dkt. Bilal, kuhutubia wananchi
wa Kijiji cha Idetero Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa, wakati wa hafla
ya uwekaji Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mradi wa Vituo vya Mapumziko na
Vyoo vya Wasafiri katika Barabara Kuu nchini, juzi Okt 17, 2015.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akisikiliza maelezo ya ujenzi huo kutoka kwa msimamizi wa Ujenzi,
Stanley Ndosite Nzowa, wakati wa hafla ya uwekaji Jiwe la Msingi la
Ujenzi wa Mradi wa Vituo vya Mapumziko na Vyoo vya Wasafiri katika
Barabara Kuu nchini, juzi Okt 17, 2015. Tuesday, 22 September 2015
Walinzi wa rais Burkina Faso ‘kupigana’
![]() |
| Wanajeshi wamelakiwa kwa shangwe na waandamanaji ambao wamekuwa wakipinga mapinduzi |
Hayo yamejiri huku marais wa mataifa ya Afrika Magharibi chini ya muungano wa Ecowas wakikusanyika Abuja, Nigeria kufahamishwa na Rais wa Senegal Macky Sall kuhusu hatua zilizopigwa katika kutatua mzozo huo.
Duru zinasema mashaurino ya kupatanisha wanajeshi hao na walinzi waliopindua serikali yaligonga mwamba usiku, suala tata likiwa hatima ya walinzi hao wa rais.
Rais Sall amekuwa akiongoza mashauriano akishirikiana na mwenzake wa Benin Yayi Boni.
Barabara za kuelekea ikulu ya rais hazina watu wala magari huku hali ya wasiwasi ikiendelea kutanda Ouagadougou.
Kiongozi wa mapinduzi Jenerali Gilbert Diendere alikuwa awali ameambia BBC kwamba yuko tayari kurejesha mamlaka kwa uongozi wa kiraia, lakini baada tu ya mpango wake wa kumaliza mzozo wa sasa kuungwa mkono na viongozi wa mataifa ya eneo hilo.
Akiongea kutoka mafichoni, Jenerali Diendere aliambia BBC: “Kuwa tayari kusalimu amri? Hatujafika huko bado …Tungependa kuendelea na mazungumzo na tunawaambia wote kwamba tuko tayari kutekeleza maamuzi ya Ecowas (kundi la mataifa ya Afrika Magharibi).”
Aidha, aliomba radhi kwa raia, akisema hilo tu ndilo wawezalo kufanya kwa sasa.
Walinzi wa rais waliopindua serikali ni watiifu kwa kiongozi aliyetimuliwa mamlakani mwaka jana Blaise Compaore.
Walimzuilia Kaimu Rais Michel Kafando Jumatano iliyopita, na kumtangaza Jenerali Diendere kuwa kiongozi mpya.
Tangu wakati huo, watu 10 wameuawa kwenye makabiliano kati ya waandamanaji wanaopinga mapinduzi hayo na maafisa wa usalama. Watu zaidi ya 100 wamejeruhiwa.
Balozi wa Ufaransa nchini Burkina Faso, Gilles Thibault, aliandika kwenye Twitter kwamba Bw Kafando ameachiliwa huru na sasa yumo kwenye makao ya balozi huyo.
Monday, 21 September 2015
MWALIMU ALIYETOWEKA MABAKI YA MWILI WAKE YAPATIKANA SHAMBANI KWA MWALIMU MWENZAKE....
Wednesday, 16 September 2015
wazazi wa luke shaw wamshuhudia mtoto wao akiumia uwanjani>> na kusema hivi

Kumbe jana usiku wakati Luke Shaw anapata jeraha kubwa ambalo litamfanya akae nje ya uwanja angalau kwa miezi 6, wazazi wake walikuwepo uwanjani kumuangalia mtoto wao akicheza mechi ile.
Bahati mbaya wamemshuhudia mtoto wao akipata maumivu makali badala ya kumuona akiisaidia club yake. Taarifa zinasema kwamba wazazi hao walishindwa kumalizia kuangalia mechi walielekea hospitali ambapo Luke alipelekwa. Siku ya leo Luke Shaw anategemea kufanyiwa matibabu kamili ili kuendelea kuuguza mguu wake.
Luke amelazwa kwenye hospitali ya St Anna Ziekenhuis ambapo Ed Woodward amemtembelea leo asubuhi.
Moreno ambae alihusikka kwenye rafu hiyo alisema, “Najiskia vibaya sana kwake najiskia vibaya snaa kwasababu najua jinsi anavyojiskia. Kitu kama kile kimewai kunitokea mimi kwenye kombe la dunia. Namtakia heri apone haraka na halikua lengo langu”
RATIBA YA MECH ZA LEO UEFA Champions League
UEFA Champions League
Wagombea wa michezo ya Olimpiki 2024 watangazwa

Maamuzi ya mwisho yatatangazwa nchini Peru katika mkutano wa kamati kuu ya Olimpiki katika kipindi cha miaka miwili ijayo.
Mwaandishi wa habari za michezo wa BBC , anasema kuwa miji miwili ambayo inapigiwa upatu wa kuteuliwa ni Paris na Los Angeles.
Bondia afariki baada ya kupigwa 'knock out'
![]() |
| David Browne |
Brown ambaye ni baba ya watoto wawili alipelekwa katika chumba cha wagonjwa mahututi kabla ya mitambo inayomsadia kuzimwa alipokosa kuimarika kiafya.
Muungano wa wahudumu wa matibabu nchini Australia umetaka mchezo wa ndondi kupigwa marufuku nchini humo kufuatia kifo hicho.
Kifo cha Browne kinajiri wiki sita baada ya mwanamasumbwi wa Queensland Braydon Smith kuzirai na kufariki kufuatia pigano la uzani wa Feather nyumbani kwake huko Toowoomba.
Hapatoshi >>>Lissu amjibu JK, Kuhusiana na SAKATA LA Richmond

MWANASHERIA mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, amemkingia kifua mgombea urais wa chama hicho, Edward Lowassa akisema hahusiki na sakata la Richmond.
Lissu ametoa kauli hiyo siku moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kunukuliwa na gazeti moja akisema kuwa muhusika wa Richmond ni yule anayetembea na Lissu katika kampeni huku akimtaka amtaje kabla Rais Kikwete hajafanya hivyo.
Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika Viwanja vya Shule ya Msingi ya Kiwanja cha Ndege Manispaa ya Morogoro jana, Lissu alimtaja kwa jina kigogo wa serikali akisema ndiye muhusika mkuu wa wa Richmond na si Lowassa.
Kauli hiyo ya Lissu haitofautiani na ile ya Lowassa aliyoitoa alipokuwa akijiunga na Chadema ambapo alisema katika moja ya vikao vya serikali vya kujadili sakata hilo, kiongozi mmoja alisema amepata amri kutoka ngazi za juu kwamba asaini mkataba wa kampuni hiyo.
Lissu alisema ni vema Watanzania kutambua kuwa mmiliki halali wa Richmond ambayo imebadilishwa majina kutoka Dowans hadi Symbion kwa sasa yupo ngazi za juu serikalini.
‘’Huyu mzee wa watu wameshampaka matope vya kutosha na wala hajatoka mbele za watu kulalamika, anatumia busara zaidi.
‘’Tunaishangaa serikali kuendelea kuwadanganya wananchi bila ya huruma kwa kudai kampuni hizo zote zinamilikiwa na Lowassa, kama kungekuwa na ukweli wowote, kwanini wanaendelea kulipa hayo madeni ya mabilioni ya fedha?
“Ni lazima Watanzania watambue kuwa Richmond ilijadiliwa bungeni ikiwa chini ya mwenyekiti wake Dk. Harisson Mwakyembe ambaye alikuwa kwenye kamati ya Bunge iliyochunguza mkataba wa Kampuni ya Richmond na mwishowe kuja kuibuka kashfa ya mafisadi ambao walikuwa 11,” alisema na kuongeza.
“Katika mlolongo wa mafisadi waliotajwa namba tisa alitajwa Lowassa wakati akiwa waziri mkuu, lakini hakuhusika moja moja na suala hilo,” alisema.
Lissu alisema katika orodha hiyo namba 10 alitajwa kiongozi mmoja mstaafu na baadae akataja tena jina la kigogo mwingine ambaye alisema huyo ndiye mmiliki wa kampuni hiyo.
Alisema Lowassa ambaye anatembea naye katika kampeni zake hahusiki hata kidogo na suala hilo ila aliwajibika kisiasa ili kuiokoa serikali, kwa kuwa alikuwa msimamizi wa serikali hiyo.
Lissu alisema ili kuondoa mfumo mbovu ni lazima wahakikishe wanaing’oa serikali iliyopo madarakani kwa kipindi cha muda mrefu, kwani hiyo ndio chanzo kikuu cha umaskini.
Lowassa: na wakulima
Kwa upande wake Lowassa, alisema serikali yake itakuwa rafiki kwa wakulima na wafugaji na kuwa atatoa elimu bora bila malipo yoyote.
“Hakutakuwa na mambo ya michango ya ajabu ajabu, tutatoa elimu ya bure lakini iliyo bora,” alisema.
Kuhusu suala la viwanda vya miwa, alisema atahakikisha viwanda vinavyowezekana vitarudishwa mikononi mwa serikali.
Alisema pia kuwa, wafanyabiashara ndogo ndogo wakiwamo mama lishe na bodaboda, atawahakikisha wanaendelea kuwa rafiki zake.
Sumaye: CCM inahukumiwa kwa uongo wake
Waziri mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye, alisema kwa sasa CCM inahukumiwa kwa kusema uongo kwa kipindi cha miaka 50 tangu taifa lipate uhuru
Alisema katika kipindi hicho, chama hicho kimeshindwa kukidhi mahitaji muhimu ya Watanzania, hivyo wananchi wamechoka kudanganywa .
Aidha Sumaye alidai Watanzania bado wamekuwa wakiishi katika mazingira magumu na yenye shida pamoja na CCM kuja na sera yake ya uongo ya maisha bora kwa kila Mtanzania .
“Ni wazi hakuna ubishi kama Watanzania sasa wamechoshwa na uongo wa CCM, ndio maana wametuunga mkono kwa asilimia 100 katika mikutano yote ya Ukawa pasipo kuletwa na magari kama ilivyo katika mikutano yao”alisema Sumaye .
Alisema uongo wa CCM unajionesha wazi wazi kwenye sekta ya kilimo, afya , miundombinu, elimu na kudai kuwa hayo ni maeneo ambayo yanawatesa kwa kiasi kikubwa na kuyaona maisha kuwa magumu.
Alisema kuwa dalili za Watanzania kuunga mkono ukawa ni dalili tosha kuonesha wanahitaji mabadiliko ndani ya taifa , pasipo kushawishika na pesa .
“Hapa mmekuja kwa upendo wenu na taifa lenu hamjaletwa kwa magari kama ilivyo katika mikutano yao (CCM),” aliongeza Sumaye .
Naye Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Kanda ya Kati wa Chadema, Mathew Likwina akizungumza na wanachama wa chama hicho alisema kuwa lengo la UKAWA ni kufanya mabadiliko ya kimfumo.
Alisema kuwa kuondoa mfumo sio kubadilisha kiongozi mmoja wa ccm , bali ni kuondoa uongozi wote wa CCM usio na mfumo mzuri katika kuleta maendeleo ya taifa na watu wake .
Aidha alidai kuwa kama Watanzania wataiondoa CCM taifa linauhakika mkubwa wa kuwa na mfumo mzuri Wenye kujali maslahi ya wananchi badala ya sasa CCM imekuwa na mifumo ya kujali watu wachache na familia zao .
NEC: Lushoto hawatapiga kura ya ubunge
![]() |
Hatua hiyo, inatokana na kufariki dunia kwa aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa mwamvuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Mohamed Mtoi (39).
Mtoi, alifariki dunia Jumamosi iliyopita baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kuacha njia na kupinduka kisha kudumbukia kwenye korongo wilayani Lushoto.
Akizungumza na MTANZANIA jana, Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva, alisema sheria inaruhusu kama mgombea atafariki dunia wakati huu wa uchaguzi uahirishwe.
“Wananchi wa Lushoto hawatapiga kura ya mbunge Oktoba 25, tumeahirisha hadi hapo baadaye tutakapowatangazia na chama husika kitapokuwa kimepata mgombea,” alisema Jaji Lubuva.
Kulingana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Zubery Mwombeji, Mtoi alipata ajali katika eneo la Magamba Coast, Kata ya Magamba wilayani Lushoto.
Alisema gari hilo lilikuwa likiendeshwa na Miraj Nuru (43), likitokea Tarafa ya Mlola kwenda Mkuzi baada ya kumaliza shughuli za kampeni.
Facebook, Kuja na mabadiliko haya wakati wowote !!

UEFA: Man United, Man City zachapwa
Timu za Uingereza za Man United na Man City zimeanza vibaya michuano ya kombe la kilabu bingwa barani Ulaya baada ya kuchapwa.
Man City nao wakiwa katika dimba lao la Etihad walikubali kipigo cha mabao 2-1 toka kwa vibibi vizee vya Turin Juventus mabao ya Juve yakifungwa na Álvaro Morata na Mario Mandzukic huku bao la kujifunga la beki Giorgio Chiellini, likiwapa Man City bao moja.
Real Madrid wakiwa nyumbani Santiago Bernabeu wameshinda kwa kishindo kwa ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Shakhtar Donetsk, Cristiano Ronaldo akifunga hat trick na Karim Benzema akifunga bao moja.
Matokeo mengine ya michuano hii ni:
PSG 2 – 0 Malmö FF
VfL Wolfsburg 1 – 0 CSKA
Benfica 2 – 0 FC Astana
Galatasaray 0 – 2 Atletico Madrid
Sevilla 3 – 0 Borussia Mönchengladbach
Monday, 14 September 2015
Jeshi la Misri ladai kuua watu 12 kimakosa
![]() |
| Kikosi maalum kimetumwa kuchunguza tukio la mauaji |
kwa upande wa Rais wa Mexico, Enrique Pena Nieto amekemea tukio hilo na kusema kuwa ameitaka serikali ya Misri kufanya uchunguzi wa kina, Wizara ya mambo ya nje ya Mexico imethibitisha kuwa takriban raia wake wawili wameuawa na kuongeza kuwa inafanya jitihada kuwatambua waathirika wengine.
tamko la wizara limesema , Balozi wa Mexico nchini Misri, Jorge Alvarez Fuentes alitembelea hospitali na kuzungumza na raia watano wa Mexico ambao hali zao zilikuwa njema.
Saturday, 12 September 2015
Serena William apata pigo kwenye mchezo wake wa Nusu fainali
![]() |
Serena katika mkutano na vyombo vya habari baada ya mechi hiyo. |
''Hili ni pigo kubwa katika historia ya mchezo huu kutokana na kile kilichofanyika''.
![]() |
Serena akisalimiana na Vinci baada ya mechi hiyo |
William alianza mechi hiyo akiwa hajashindwa katika mechi 33 katika Grand Slum tangu machindano ya Wimbledon ya mwaka 2014.
Alikuwa amejitahidi kufikia rekodi iliowekwa na Steffi Graf ya mwaka 1988 ambapo mwana dada huyo alizoa mataji yote mwaka huo na alikuwa akikabiliana na mchezaji ambaye alimshinda mara nne bila kushindwa seti moja.
Thursday, 2 July 2015
Ugiriki yaonywa kuhusu kura ya 'La'
![]() |
| Raia wamegawanyika huku wengi wakianza kuhamia kambi ya 'Ndio' |
Hofu ya Ebola DRC
![]() | |
| Mgonjwa wa Ebola DRC |
Boko Haram yashambulia zaidi
![]() |
| Boko haram wazidisha mashambulizi |
Habari zinasema pia wanaume 48 wamepigwa risasi na wapiganaji katika mashambulizi tofauti siku ya Jumanne.
Mashuhuda wanaokimbia eneo lililopo karibu na Ziwa Chad wanasema idadi kubwa ya wapiganaji wamevamia vijiji vitatu ambapo wameuwa wanaume, wanawake na watoto.
Baadhi ya ripoti zinasema walipigwa risasi huku wengine wakielezea jinsi wapiganaji hao walivyowachinja watu na kuchoma majengo.
Upande wa Kusini, nje kidogo na mji wa Monguno, kundi la wapiganaji wa Boko Haram wamefika usiku wakati watu walipokuwa wanaswali. Waliwasubiri mpaka walipomaliza kuswali na kuwatenganisha wanaume na wanawake na baadae kuanza kuwamiminia risasi wanaume.
Mwanasiasa anayewakilisha eneo hilo, Mohammed Tahir amesema awali alitoa tahadhari kwa jeshi la Nigeria kwamba vijiji hivyo viko hatarini kwa sababu Boko Haram wameweka makazi katika maeneo hayo baada ya kutimuliwa katika himaya yao ya msitu wa Sambisa.
Haya ni mashambulizi mabaya zaidi kufanywa na Boko Haram katika kipindi cha wiki kadhaa.
Kundi hilo limekuwa likilipuwa mabomu kadhaa baada ya kudhoofishwa na majeshi ya Nigeria.
Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari amesema kipaumbele chake ni kuimarisha mapambano dhidi ya Boko Haram.
Msumbiji yakubali mapenzi ya jinsia moja
![]() |
| Nchi chache Afrika zimekubali mapenzi ya jinsia moja |
Hata hivyo nchi nyingi za Afrika zimeweka sheria kali dhidi ya mapenzi ya jinsia moja.Nigeria ilipiga marufuku na kuweka adhabu ya kifungo cha miaka 14 jela kwa wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.Uganda nayo imeapa kurejesha sheria kali kuharamisha mapenzi ya jinsia moja.
Sheria ya awali ilitupiliwa nje na mahakama ya kikatiba.
Msumbiji sasa anajiunga na mataifa mengine ikiwa ni pamoja na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Ivory Coast na Afrika Kusini ambapo siyo hatia kuwa mpenzi wa jinsia moja.
Vikwazo kwa makamanda wa S Sudan
BREAKING NEWS-Bunge Laharishwa gafla baada ya Wabunge wa UKAWA kugomea Miswada Petroli na Gesi

Ni baada ya John Mnyika kuomba Muongozo juu ya uvunjaji wa kanuni za bunge. shuguli za leo zimekiuka kanuni kwani miswada imewekwa ikiwa sambamba. anasema hoja ikishatolewa ni lazima ijadiliwe iamuliwe ndo itolewe hoja nyingine, lakini leo zipo hoja tatu kwa pamoja.
Mnyika kasema na huu Muongozo sitaki useme utautolea ufafanuzi siku nyingine kwa maana hatuwezi kuendelea kufanya kazi ambazo zimevunja kanuni.
Wanapinga kuwasilishwa kwa dharula na kwa pamoja Miswada yenye manufaa makubwa kwa nchi.
Miswada wanayo pinga na iliyo wasilishwa kwa pamoja ni;
1.Muswada juu ya Petroli, 2015 (The Petroleum Act, 2015):
2.Muswada juu ya Usimamizi wa Mafuta na Gesi, 2015 (The Oil and Gas Revenues Management Act, 2015):
3.Muswada juu ya tasnia ya Uziduaji Tanzania (The Tanzania Extractive Industries Act, 2015): The Tanzania Extractive Industries Act, 2015.
Hata baada ya Spika kuwataka watoke nje kama hawataki kuendelea, Wamegoma na kusimama na kuanza kupiga kelele hadi Spika akaahirisha bunge. UKAWA wamesema mwanaharamu hapiti leo.
Chadema yaibwaga CCM mahakamani
Upinzani wambana Dk Migiro, AG bungeni
![]() |
| Waziri Kivuli wa Sheria (Chadema), Tundu Lissu akichangia muswada wa Kuwalinda Watoa Taarifa za Uhalifu na Mashahidi wa mwaka 2015 bungeni mjini Dodoma jana. |
Malumbano ya wawili hao yalianzia pale Mnyika aliposema kuwa Serikali ni dhaifu katika suala zima la utungaji wa sheria jambo ambalo pia liliamsha hasira za Spika.



























