Wednesday, 17 September 2014

ARSENE WENGER ANENA KUHUSIANA NA WELBECK KUPOTEZA NAFASI ZA MAGOLI DHIDA YA BORUSSIA



Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amefunguka kuhusiana na suala la mshambuliaji wake mpya Danny Welbeck kupoteza nafasi katika mechi dhidi ya Borussia Dortmund.


Wenger amemkingia kifua Welbeck ambaye alipoteza nafasi zaidi ya mbili katika yake ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa na Arsenal.
Welbeck alinunuliwa na Arsenal kwa pauni milioni 16 akitokea Manchester United.
Tokea jana usiku, amekuwa gumzo kwenye mitandao wadau wakionyesha kuchukizwa naye kupoteza nafasi huku Arsenal ikiambulia kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Wajerumani hao.

0 comments:

Post a Comment