Thursday, 22 January 2015

Mkoa wa KIGOMA watakiwa kumaliza mgogoro wa Ranchi ya UVINZA

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt TITUS KAMANI

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt TITUS KAMANI ameuagiza uongozi wa mkoa wa KIGOMA kuhakikisha mgogoro wa mpaka kati ya Ranchi ya Uvinza na pori la Akiba la Moyowosi unakwisha mara moja na ametaka pia uonevu unaofanywa dhidi ya wawekezaji wa mifugo katika ranchi ya Uvinza ukome mara moja.

Waziri KAMANI ametoa agizo hilo kufuatia malalamiko ya wawekezaji wa mifugo waliopewa vitalu katika RANCHI ya Uvinza kuwa wamekuwa wakichomewa mazizi ya mifugo yao, nyumba za watumishi , kuporwa mifugo yao kupigwa na kulazimishwa kutoa fedha na baadhi ya watumishi wa kampuni iliyopewa kitalu cha kuwinda katika pori la Akiba la MOYOWOSI wilayani KASULU

0 comments:

Post a Comment