Thursday, 22 January 2015

Kituo kingine cha Polisi kuvamiwa na Majambazi Tanzania

Polisi Ikwiriri
Msemaji wa Jeshi la Polisi Bi Advera Bulimba
Askari wawili wa kituo cha Ikwiriri wilayani Rufiji mkoani Pwani wameuawa na majambazi ambao idadi yao haijafahamika ambao baada ya kufanya mauaji walipora bunduki tano, risasi 60 na mabomu mawili ya machozi ndani ya kituo cha Polisi.

Walikuwa ni majambazi wengi, walivamia na kuanza kuwashambulia askari wetu, walifanikiwa kuwaua askari wetu wawili na kuchukua silaha… Polisi imelaani tukio hilo, msako mkali umeanza na milioni 20 itatolewa kwa atakaefanikisha Majambazi hawa kukamatwa“– Advera Bulimba, msemaji wa Jeshi la Polisi akiongea on ITV

Majambazi hawa walivamia wakiwa na silaha za moto, mabomu ya kurusha kwa mkono na mapanga ambapo hili linakuwa tukio jingine kulisikia baada ya lile la Majambazi kufanya vivyo hivyo kwa kituo cha Polisi Geita.

0 comments:

Post a Comment